#HABARI: Shirika la Afya Duniani (WHO), limetangaza mlipuko wa ugonjwa wa mpox (Homa ya Nyani) katika baadhi ya nchi za Afrika, kuwa dharura ya afya ya umma ambayo inaleta hofu kimataifa.
Ugonjwa huo unaoambukiza kwa haraka umeshaua takribani watu 450 tangu ulipuke katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, ambapo ugonjwa huo unaelezwa kuenea katika maeneo ya Afrika ya kati na mashariki, huku wanasayansi wakiwa na wasiwasi kuhusu jinsi aina mpya ya ugonjwa huo inavyoenea na kiwango chake cha juu cha vifo.
Whatsapp
https://chat.whatsapp.com/Kdbqqe1TWCn10djL2rnQBC

Comments
Post a Comment