HALI ZA KAWAIDA ZA SEHEMU ZA UKENI
Je Kutokwa na Uchafu Wa Ukeni Wa Kawaida ni nini?
Wanawake wote hutokwa na uchafu ukeni, ingawa kiwango hutofautiana. Wakati mwingine ni nzito, au nyepesi, au hata
haionekani. Wanawake waliokomaa hupata uchafu huu kwa kiwango kidogo sana. Hutegemea ikiwa mwanamke anapata hedhi au kama anatumia vidonge vya kuzuia mimba.
Uchafu huu huweka uke wa mwanamke kuwa na afya nzuri ingawa wakati mwingine huweza kuleta shida.
Nitajua Vipi lkiwa Niko Na Maambukizi Katika Uke Wangu?
Unaweza kutambua ikiwa uko na dalili hizi.
• Kujikunakuna, kuchomwa au hata uvimbe kwenye uke.
• Uchafu huwa unatoka kwa wingi na kisha unasababisha harufu mbaya.
• Wakati wa kukojoa unahisi uchungu.
• Uchungu wakati wa ngono.
Iwapo utakuwa na dalili hizi basi muone muuguzi au mhudumu wa upangaji uzazi.
Naweza Kufanyaje li Kuweka Uke Wangu Kuwa wa Hali Safi Na ya Afya?
Kuna mambo mbalimbali unayopaswa kutekeleza.
• Tumia chupi iliyotengenezwa kwa pamba au chupi ambayo haitakuchoma na kubadilisha chupi kila siku.
• Pia usivae soksi au suruali ndefu ya kubana kwa mda mrefu.
• Osha chupi kwa maji moto na sabuni kisha ukamue chupi hizo kwa maji masafi kabla ya kuanikwa.
• Badilisha nguo zenye unyevunyevu baada ya kuogelea au nguo za michezo baada ya mchezo bila kukawia.
• Tumia visodo badala ya taulo. Badilisha taulo mara kwa mara. na usitumie zile za marashi.
• Usivalie nguo za kukubana kwa sababu zinafanya mwili kuwa na unyevu na kisha husababisha vidudu kusambaa kwa haraka.
• Epuka kuosha uke kwa kutumia sabuni zenye manukato au mbinu yoyote ile kwa sababu huongeza kujikuna. Uke wenye afya hauhitaji marashi au manukato.
• Jiepushe na matumizi ya sabuni, chumvi za kuoga na manukato katika maeneo haya.
• Tumia sabuni ya kawaida na maji katika maeneo haya.
• Panguza kutoka mbele hadi nyuma baada ya kujisaidia kuepusha uchafu kugusa maeneo haya.
• Usitumie shashi zenye manukato.
Wakati mwingine dalili hizi zaweza sababishwa na mambo mengine makubwa, kwa hivyo hakikisha umemwona dakitari.
Kwa kuongea na dokta wetu bofya Link ya whatsapp hapa chini
Message Afya bora on WhatsApp. https://wa.me/255774039825
Kwa maelezo zaidi:
+255 626 908 654
+255 718 958 410

Comments
Post a Comment