PID NI UGONJWA GANI.?
Ugonjwa wa PID Hauwezi Mpata Mwanaume Bali Mwanaume Anaweza kumwambukiza Mwanamke Ugonjwa huu wa PID.
Maambukizi ya via vya uzazi vya mwanamke au ugonjwa wa PID "Pelvic inflammatory disease" Ni maambukizi ya bacteria kwenye Shingo ya uzazi, Mirija ya fallopia, Ovari na Tumbo la uzazi (Uterusi).
Sababu kuu ya ugonjwa huu wa (PID) ni maambukizi yanayo sambazwa kwa kujamiiana (STIs).
Dalili za ugonjwa huu wa (PID) huweza kujumuisha, Maumivu ya nyonga, Maumivu ya tumbo chini ya kitovu, Maumivu wakati wa tendo la ndoa, Homa kali, Na uchafu mzito mweupe na wenye harufu mbaya kutoka ukeni.
Utambuzi wa ugonjwa huu hufanywa kulingana na dalili na uchunguzi wa sehemu za siri, Katika uchunguzi wa kitaalamu sampuli za majimaji au usaha huchukuliwa ili kutambua bacteria aliye pelekea maambukizi hayo.
Maambukizi ya via vya uzazi vya mwanamke (PID) hutibiwa kwa antibiotics, Kumbuka kwamba tiba ya ugonjwa huu hutofautiana kulingana ukali wa maambukizi, Hivyo basi usi kariri dawa,
Ikiwa maambukizi nikali itahitajika kupatia tiba ya antibiotics kwa sindano nasio vidonge tena. Kama maambukizi yamepelekea usaha kukusanyika, Uvimbe na makovu kwenye mirija ya uzazi (Fallopian tube) Upasuaji utakuhitajika.
Fahamu kwamba watu wengi hupona vizuri kabisa baada ya matibabu sahihi na maambukizi hayapelekei matatizo ya muda mrefu,
Ikiwa sasa haujazingatia tiba vizuri maambukizi yakajirudia, Au kutopatiwa tiba kabisa basi kuna uwezekano mkubwa wa kupata madhara zaidi. NA hata kupelekea mwanamke kuwa mgumba, Kutopata kabisa mtoto na Mvurugiko wa homoni mwilini.
Njia muhimu ya kuzuia maambukizi ya via vya uzazi vya mwanamke ni kuepukana na wapenzi wengi, kutumia kinga wakati wa tendo, Endapo kama umegundulika na maambukizi ya (STIs). Nimuhimu kupatiwa matibabu pamoja na Mwanaume wako.
ZINGATIA AFYA 
Kwa kupata matibabu wasiliana nasi.
+255 626 908 654

Comments
Post a Comment